Monday, November 9, 2020

KUSUDI LA MUNGU KWA MWANADAMU

 KUSUDI LA MUNGU KWA MWANADAMU

1:1UUMBAJI WA MWANADAMU

Kusudi la Mungu kumuumba mwanadamu lilikuwa mwanadamu Atawale vitu vyote Duniani. Ambapo Mungu alimwamuru mwanadamu ale wanyama na kila kitu alichokifanya Duniani. Lakini piah Mungu alitaka mwanadamu amsifu na kumwadu. mwanadamu ilimpasa kumtumikia Mungu akilinda vitu vyake alivofinya kwa mkono wake duniani.

 Biblia inasema  Mungu alipomuumba mtu bado miche ya kondeni wala mboga ya kondeni ilikuwa haijachipuka bado, kwa maana Bwana Mungu alikuwa bado hajainyeshea nchi mvua wala hapana mtu wakuilima aridhi.Basi Mungu alipanda Bustani upande wa mashariki ya Edeni akumweka mwanadamu humo.mwanzo2:4-10

Mungu alimuumba mtu mfano wake mwenyeww ambeye wa kwanza mwanamume aliitwa Adamu na wa pili alitoko ubavuni mwa Adamu ambaye alikuwa mwanamke aliitwa Hawa. Wote hawa wawili walikuwa wakiishi katika bustani ya Edeni.Mwanzo2:2125  Lakini Bwana Mungu alimwagiza mtu akisema  matunda yote utayala isipokuwa mti wa ujuzi wa mema na mabaya usiyale wala usiyaguse maana siku utakapokula hakika utakufa.mwanzo2:16-17


MWANADAMU KUONDOKA KWENYE  KUSUDI LA MUNGU

Biblia inasema basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu. Akamwambia Hawa ati Mungu ndo alivosema msile matunda ya miti ya bustani?. Mwanamke akamjibu nyoka, matunda ya miti yote twaweza kula isipokuwa matunda ya mti wa katikati Mungu amesema msiyale wala msiyaguse msije mkafa.

Nyoka akamjibu mwanamke hakika hamtakufa ,kwa maana Mungu anajua kwamba mkiyala hayo matunda mtafumbuliwa macho nanyi mtakuwa kama Mungu mkijua mema na mabaya. Mwanzo3:1-5

JAMBO LA KUJIFUNZA

Usimruhusu shetani ukampa nafasi ya kuzungumaza kama Hawa alipomruhusu nyoka kusema naye. Usitoe siri zako wewe na Mungu kwa kila mtu kama Hawa alipo eleza mambo yake yeye na Mungu na kumpa ibilisi shetani nafasi.

Wengi wetu tumeshindwa kujizui kuongea mambo yetu ya siri hata tumempa ibilisi nafasi kujua mambo yetu.Basi tambua kwamba unapotoa siri zako kwa rafiki zako huwezi jua undani wake hata kama unasali nae. Unaweza ukajikuta unakumbana na matatizo na vita isiyo isha kulingana na kuumpa ibilisi nafasi na kutambua kusudi la Mungu kwako. 

MADHARA YA KUONDOKA KATIKA KUSUDI LA MUNGU

 Laana                                                       Mtu alilaaniwa na Mungu na Mungu baada ya kutoka kwenye kusudi lake Bwana Mungu.   Kwamba Mungu alimwambia umelaaniwa kuliko wanyama wote wa mwitu. Mwanzo 3:13-19

LAANA ni hali ya kukataliwa, mtu asiye na kibari  mbele za watu na Mungu piah.                                    

 KUNA NINI KATIKA LAANA

-Huleta maadui kuongezeka juu yako.

- Aridhi itakukataa wala hutaona mafanikio katika maisha yako. mwanzo4:12

-Utakuwa ni mtu asiyekuwa na makao duniani. Mwanzo4:14

-Utakuwa ni mtu aliye hesabiwa kifo. Mwanzo 3:19

-Ni  mtu asiyekubarika na watu kila akuonae hutapata kibali mbele yake. Mwanzo 4:14.     


MAMBO YA KUFANYA ILI UFIKIE KUSUDI LA MUNGU

  • Kutenga mda wa kusoma neno la Mungu . Ili kujua nini Mungu anakusudi gani kwako,lazima uwe mtu wa neno.Yoshua 1:8
  • Ni lazima tuachane na kweli za dunia.kweli za dunia ni kweli alizotumia shetani kumdanganya Hawa kwamba hautakufa ila utajua mema na mbaya. Jambo hili lilimkosesha Hawa Kuishi katika kusudi la Mungu.                                            

-Mfano wa kweli za dunia.

-Mbona unajitengatenga na wezio itakuwa kama mtu asiye na mahusiano muzuri utaone kana  kama unashida

-Ukiwa na mke mmoja utapata baadhi ya magonjwa ya kiume.(tezi dume)

-Binti au kijana usipotongoza au kutongozwa wewe utakuwa na matatizo.

Hizo ni kweli za duniani wala sio kusudi la Mungu.

  • Kutenga mda wa Maombi ,ni vizuri kuwa na mda wa kumuomba Mungu . Bibliabinasema kesheni mkiomba msije mkaingia majaribuni Luka 22:40-46
  • Lazima  umjue na kumwamini unayemtumikia na kumwelewa viđź‘€zuri.Yohana 14:10.

Mungu wa mbinguni akubariki


Sunday, November 8, 2020

KUMTUMIKIA MUNGU

 KUMTUMIKIA MUNGU 

MAMBO YATAKAYO KUSAIDIA KUMTUMIKIA MUNGU. 

1-Nguvu ya Roho mtakatifu

Roho mtakatifu ni ahadi kwa kila mwamini ambayo Yesu alimwahidia mwanadamu.(Yohana16:7-16)

 Roho mtakatifu hukaa kwa watu walio amini ya kuwa Yesu ni Bwana na mwokozi wa maisha yao na kubatwiza.         Lakini pia tunaona Yesu anawaagiza wanafunzi wake wasitoke Yerusalemu waingoje ahadi ya Baba ambayo ndiye Roho myakatifu .

Mungu hapo mwanzo aliwapa watumishi wake Roho mtakatifu kulingana na kazi ambayo anataka ifanyike. Roho mtakatifu alikaa na manabii  tunaona Nabii kama Eliya Mungu  alimpaka mafuta kupitia Roho mtakatifu ambeya alimwongozo katika kutumika pamoja na Mungu.

KAZI ZA ROHO MTAKATIFU 

  • Roho mtakatifu hutuosha dhambi zetu .  Biblia inasema Yohana alibatiza kwa maji lakini Yesu atawabatiza kwa Roho mtakatifu. Ndo maana Roho mtakatifu hukaa na watu walio wasafi wa moyo na yeye hujuza matendo mema.      Matendo 1:5,mathayo3:1-12 
  • Roho mtakatifu hufanya kanisa kuongezeka kupitia ushudiaji. Ukitumika pamoja Roho mtakatifu yeye ndo atafanya ushudiaji ndani ya mioyo ya watu. (matendo2:37-42)
  • Roho mtakatifu hutupa ujasiri katika kumtumikia Mungu. Roho mtakatifu alimpa ujasiri Petro kunena maneno ya Mungu baada ya kupata Roho mtakatifu (Matendo1:8)
  • Roho mtakatifu hutupaka mafuta.    Roho mtakatifu hutupa mafuta kwa ajili ya kutumika kama Mungu alivowapaka mafuta watumishi wake katika agano la kale.(    Luka3:21-23)
  • Roho mtakatifu hutupa umoja.   Matendo2:43-47.      Roho mtakatifu hutupa umoja wa kimungu maana yeye ni Mungu. Kanisa linalo ongozwa na Roho mtakatifu ni kanisa lenye upendo na ushirika mzuri.
  • Roho mtakatifu hutuongoza.  (Matendo19:6 ), Jifunze kumtumia Roho mtakatifu kwa kusikliza sauti yake na kuitambua Roho mtakatifu hutuonya mara kwa mara likini tumeshindwa kutafsiri.
  • Roho mtakatifu hutupa maono. (Matendo2:16-18,Yoeli2:28-32)Mungu anasema itakuwa siku mwisho nitamwagia watubwote Roho yangu na wana wenu wataona maono na wezee wenu wataota ndoto.

Saturday, November 7, 2020

KUMTUMIKIA MUNGU

KARIBU TUENDELEE NA SOMO LETU (katika umtumikia Mungu)

 Tumeona hapo mwanzo nini maana ya kumtumikia Mungu, likini sasa lazima utambue pia kwamba kuna gharama katika kumtumkia huyu Munngu. Tunamwona Yesu mwenyewe alivo pata shida katika kueleza kusudi lake la kuja duniani /naweza kusema kueneza injili kwa wana wa israeli. Ambalo lilikuwa kusudi kila mwanadamu apate injili kama hivi leo.

 Ukisoma biblia( Mathayo 13:54-58) Tunaona Yesu alivopata shida kueneza injili katika nchi yake mwenyewe ambapo watu walimtumbua Yesu kama mtoto wa selemala na waliitambua vyema familia yake Yesu hata hawakuamini mafundisho yake  wala kazi zake inasemekana hakufanya miujiza mingi katika nchi yake mwenyewe watu wengi wa kwenu hawata kuamini.

Kuna watu unaweza kutana nao wanajua injili kuliko wewe,wanaijua biblia sana lakini hawatambui nini maana ya wokuvu ni watu wa dini tu.Tunamwona Yesu alikutana na watu walioshika dini tangu kwa mababu zao wanazijua sheria sana. Lakini Yesu anasema ni watu walioyoshika mapokeo ya wanadamu(Marko 7:1-7)(mstari wa saba unasema  nao waniabudu bure,wakifundisha mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu).

Basi ukitaka kumtumikia Mungu lazima ujikane mwenyewe na kujitwika msalaba wako mwenyewe. Haijalishi ni magumu gani utakumbana nayo utapitia taabu mbalimbali ukizani Mungu amekuacha lakini usikate tamaa Mungu yu pamoja nawe. 

 Tuchukue mfano wa biblia Yohana alifungwa gerezani na Yesu alikuwa akifufua watu na viweta walitembea na vipofu kuona lakini mtumishi wa Mungu Yohana alikuwa amefungwa gerezani wala asifanye muujiza kwake wa kumtoa gerezani(Mathayo11:1-7).

Tunaona hata Yohana mwenyewe anatuma wanafunzi wake wamfuate Yesu na kumuuliza ni wewe masihi ama tumtarajie mwingine ,Yesu anajibu mwambieni vipofu wanona viwete wanatembea, kwanini basi hakumtoa gerezani . Kumbe ilimpasa mtumishi wa Mungu Yohana afe kuwa ushuda wa kutumika pamoja na Mungu, kwamba imetupasa mateso kwa ajili ya watu wengine ili waokolewe. 

Kumbuka:

Kumtumikia Mungu kunahitaji 

1-Uwe msafi wa moyo nikimaanisha kwamba uvae drii ya haki kifuani mwako. Drii ya haki ni kuwa mtakatifu ili uombapo haja zako mbele za Mungu zisikike na zijibiwe piah.(waefeso6:14)

Wengi wetu tumejichanganya katika mambo yetu wenyewe kwa kutegemea akili zetu wenyewe huku tukisubiri kijibiwa haja zetu hali kwamba wajua siri za moyo wako.

2-Uwe mwaminifu ;Mda mwingi tumekosa uaminifu mbele za Mungu na mbele za rafiki zetu lakini kumbuka mwanadamu mwenzio hakuoni lakini Mungu anakutazama kwa jicho la karibu sana, ( maana biblia inasema macho yake Mungu yapo duniani kuwangalia watenda mema na mabaya).

3-Uwe mtu wa ibada ; naweza kusema mshumaa wawezaja kusimama wenyewe bila kuwekewa kishikizo. Mti wawezaje kusimama bila mizizi  ndivo na wokovu lazima uwe na sehemu ya kujishikiza .Nilazima uwe mtu wa sehemu ya ushirika ili uweze kusima. Biblia inasema imani chanzo chake ni kusikia kumbe nilizima kuwa mtu unayependa kusikia maneno ya Mungu. Tunaona ushirika wa kanisa la mitume wa Yesu walivofanya mambo kwa ushirka na kwa upendo walifanikiwa sana!!( Matendo 2:42,)

Tumeona watu wengi wanaokoka ni baada ya kupata ushuda ambao unawajengea imani ndani yao ya kwamba Mungu yupo na anaweza.

4-Lakini pia ni lazima uwe mtu mwenye ushuda mzuri mbela za watu au jamii inayokuzungu ili wakunenee mema na mambo ya hekima yaje kwako. 

Sio mtu unaye sifika kwa mambo ya giza kama uzinzi mtu wa masengenyo mtu watabia za kubeba wake za watu mtu wa kubeba waume za watu mtu wa kubeba binti za watu. Wasikuambie twende tukafanye ushudiaji mtaani kwako ni mtu umejaa hofu ya maovu yako unayoganya huko umeifanya kazi ya Mungu ngumu.Tengeneza ushuda mzuri watu wakutambue.

5-Jambo la tano ni kumtambua unaye mtumikia.  Maran wakristo tumefanya mambo kwa mazoea kanakwamba Mungu ni jamaa mmoja tu hivi tunayemfahamu lakini sio kwamba ni Mungu ambaye anapaswa kusujudiwa.

Napenda nikwambie kwamba mtambue Mungu kama ni mfalme katika maisha yako yote maana biblia inasema ni Mungu aliye na kiti cha ufalme mbinguni . Inatupasa kumweshimu Mungu kwa kumsujudia. 

MUNGU ANASEMA YEYE NI MUNGU MWENYE WIVU NA OLE WAKE ALITAJAYE JINA LAKE BURE

KUTOKA 20:7(Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako,maana BWANA hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure). 

Wengi ni wahubiri wakubwa lakini tumelitaja jina lake Mungu bure! 

Hayo ni mambo machache ya kuyajua ili ili Mungu akutumie katika maisha yako, Tamani kumtumikia Mungu ili awe karibu na wewe. Wengi tumeshindwa kuwa na kiu ya kumtafuta Mungu ndo maana hatuja muona Mungu katika maisha yetu. Mungu anataka watu walio na kiu ya kuutafuta uso wake ili awaonyeshe ukuu wake!! 

KUNA  MAMBO MENGI YAMETUNGE NA USO WA MUNGU

1-Tamaa ,tamaaa ni adui wa haki katika maisha yetu hasa kwa mkristo ni jambo kubwa ambalo limetukosesha sana kumwona Mungu.                                Kwanza kabisa ni: Usinzi ,Fedha . (Waefeso5:3-5).

  • Wengi wetu tumetamani kuwa na vitu vingi vizuri mwanamke mzuri , magari, majumba mazuri. Lakini kumbuka kwamba kuvipata vitu hivi ndo kunaongeza tamaa kwa mwanadamu tunamwona sulemani alipopata mali nyingi ilimpa  kiburiya kuoa wanawake wengi ambapo pia ilipelekea kumweka mbali na uso wa Mungu .     Yote ni kwasababu yalimpelkea kuenenda katika njia zake mwenyenyewe na kuabudu sanamu (1wafalme11:1-7).

Lakini pia Yakobo anasema Mungu hamjaribu mtu maana yeye hawezi kujaribiwa na maovu ,lakini tunajiletea majaribu wenyewe kwa tamaa zetu huku tukivutwa na kudanganywa(Yakobo1:12-16).

2-Maisha ya kidunia ,wengi wetu tumesumbukia maisha yetu wenyewe kuliko mambo ya Mungu. Ndo maana hatujamuona Mungu akifanya kwetu na mda mwingi tumekuwa watu wa kulalamika kila wakati.(Mathayo6:25-34).   Bali utafuteni kwanza ufalme wa Mungu hayo Mengine mtazidishiwa. 


Usisite kutoa maoni kwenye box hapo chini . Lakini piah somo nimwendelezo nakuomba jitahidi tumalize   pamoja mimi  nakuombea akupe Mungu akupe ufahamu uzidi kuyapambambanua haya!

 Ubarikiwe na BWANA.

Saturday, October 31, 2020

KUMTUMIKIA MUNGU

 UJIO WA YESU KRISTO ULIMWENGUNI

Kumtumikiia Munguni  kushiriki mateso pamoja na Yesu kristo pale msalabani.    Kuzaliwa kwa Yesu kusudi ni kumtoa mwadamu katika maisha ya kale maisha ya dhambi. Kifo cha Yesu kilidhihilisha ukombozi kwa mwanadamu kwamba Yesu alikufa na kufufuka siku ya tatu na anasema yeye ukimkubali ukanywa damu yake na na kula mwili wake utaupata uzima wa milele.     ( Yesu hakumaanisha kwamba umle yeye naunywe damu yake bali alitaka umkubali yeye kwamba ametumwa na baba ulimwenguni kwa ajili ya ondoleo la dhambi zetu ).Lakini piah kifo cha Yesu kinatupa uhakika kwamba kufa kwetu ni kuishi kwetu kwamba Yesu alifufuka basi nasi siku ajapo Yesu tutafufulia na kuishi tena tena katika makazi mapya ambayo ni Yerusalemu mpya.

Ilimpasa Yesu afe ili kuokoa wengine , kwamba ilipasa Barabara afunguliwe ili Yesu asulubiwe msalabani( Marko15:6-15) . Pia Yesu alimwambia Petro akesama nenda nyuma shetani maana huyawazi ya Mungu ila ya wanadamu, kwa maana petro alitamani Yesu asife abaki pamoja nao lakini huo haukuwa mpango wa Mungu, Yesu kubaki na wanadamu,(Marko 8:33).

Lakini piah kuja kwa Yesu na kuondoka kuna tupa sisi kazi ya kufanya kama alipo waagizi wanafunzi wake ama mitume wa Yesu kwamba amewaachia mamlaka ya kuponya wagonjwa na kila atakaye kula kitu cha kufisha na kung'atwa na nyoka hatadhulika ,Marko 16:14-20.

Lakini pia anasema aliacha vipawa kwa wanadamu pale alipo paa kwenda mbinguni ambapo aliacha wengine kuwa 

1-walimu

2-mitume 

3-wainjilisti

4-manabii

5-wachungaji

Yote ni ili kuujenga mwili wa kristo Yesu . Kumbe inatupasa kuifanya kazi ya Mungu katika maisha yetu yote ili kutimiza ujio wa Yesu ulimwenguni. Inatupasa kuihubiri injili ya Yesu kwa kila kiumbe na kubatiza kama agizo la Yesu kwa mitume pale Yerusalemu.

KUSUDI LA MUNGU KWA MWANADAMU

  KUSUDI LA MUNGU KWA MWANADAMU 1:1UUMBAJI WA MWANADAMU Kusudi la Mungu kumuumba mwanadamu lilikuwa mwanadamu Atawale vitu vyote Duniani. Am...